Kituo cha Biashara cha Kimataifa (ITC) na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) kupitia ubunifu wa Farwell walitengeneza mfumo huu ili kukabiliana na mahitaji makubwa kutoka kwa maelfu ya wafanyabiashara wadogo na wa kati, watoa huduma za kifedha na wafadhili wa maendeleo ya biashara waliofanyiwa utafiti katika Afrika Mashariki mwaka 2019 na 2020. Mfumo huu umetengenezwa kwa msaada wa kifedha wa mpango wa pili wa kuboresha upataji wa soko wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (MARKUP II) unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) na kutekelezwa na Kituo cha Biashara cha kimataifa (ITC). Usaidizi huu umetuwezesha kupanga, kuzindua, kujaribu na kulipia gharama za awali za kuwezesha mfumo kupatikana mtandaoni.